Sababu Halisi ya Chris Brown Kumdiss Rihanna Yagundulika
Imebainika
 kuwa Chris Brown alikuwa anataka kurudiana na Rihanna huku akiendelea 
na uhusiano na mpenzi wake wa sasa Karrueche Tran, kitu ambacho Rihanna 
alikikataa.
Licha
 ya wasanii hao kushirikishana kwenye remix za nyimbo zao mapema mwezi 
uliopita, mambo yaligeuka tena baada Chris kudaiwa kumtukana Rihanna 
kwenye wimbo.
Chris alipenda warudiane na Rihanna lakini wakati huo huo alikataa kumwacha Karrueche.
 Hatimaye
 Rihanna alimwambia Chris Brown kuwa anataka kuanzisha uhusiano na mtu 
mwingine kama (Chris) hatoweza kuchagua kusuka ama kunyoa.
“Chris
 hakuwa tayari kuukatiza uhusiano wake na Karrueche, japokuwa alimfanya 
Rihanna aaminini kuwa alikuwa bado akimpenda sana,” chanzo kimoja 
kimeuambia mtandao wa Hollywood Life.
“Chris
 ndiye aliyekuwa wa kwanza kumfuata Rihanna na kumuomba msamaha. 
Alionesha mahaba mazito kwake wakati akimbembeleza na kumwambia namna 
alivyommiss, jinsi asivyoweza kumfananisha Karrueche na yeye na namna 
anavyotaka kusawazisha mambo.”
 Chanzo
 hicho kiliendelea kusema “Chris wanted to have his cake and eat it 
too!” Once Rihanna made it clear that she wouldn’t stand to be his side 
chick, Chris dissed her.”

