|

Mr Nice apewa shavu na ubalozi wa Mexico

Tangu producer Lamar amrudishe hewani na TABIA GANI Lucas Mkenda aka Mr Nice mambo yanazidi kumnyookea mhasisi huyo wa style iliyokufa ya TAKEU. Wengi walikuwa wanaamini kuwa baada ya kukaa kimya kwa zaidi ya miaka mitano mwanamuziki huyo asingeweza kurudi tena lakini mambo yamegeuka kuwa tofauti. Na sasa akiwa tayari na albam yake mpya iitwayo TABIA GANI, Mr Nice amepewa ahadi nono na ubalozi wa Mexico nchini Tanzania kupromote albam yake. Hiyo ni baada ya kuyarudia mashairi ya wimbo uitwao El Rey ulioimba na msanii wa Mexico Jose Alfredo Jimenez.

Posted by Unknown on 12:53 PM. Filed under , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0. Feel free to leave a response

Blog Archive

Labels

Recently Commented

Recently Added