|

Diamond Apagawisha Songea-Show Yavunja Record


SHOO ya  nyota wa muziki wa kizazi kipya Bongo Naseeb Abdul 'Diamond' imeingia katka kitabu cha matukio yaliyokusanya watu wengi zaidi katika historia ya mji wa songea  na mkoa wa Ruvuma kwa ujumla.

Akizungumza na Teentz.com mapema leo Mkurugenzi wa Jambo Lee Club  ambayo iliratibu ziara nzima ya mwanamuziki huyo amesema kuwa shoo ya Diamond imevunja rekodi na kuingia kwenye kumbukumbu za watu  kwa kujaza watu wengi na pia  ikiwa ni shoo pekee iliyokuwa na msismko mkubwa  kuliko hata inavyokuwa  wakati wa michezo ya soka inayozihusisha timu kubwa na Simba na Yanga zinapokuja kucheza Songea.
"Shoo imefunika hakika haijawahi kutokea, watu kujaa kwa wingi kiasi kile katika  shoo za muziki hii imevunja rekodi, kwa kweli kama waratibu tumefarijika sana kuona  watu wamejitokeza kwa wingi, kwani hatukutegemea ingawa msisimko uliokuwepo kabla ulikuwa mkubwa kuliko hata ule unaokuwepo wakati Simba na Yanga zikija kucheza hapa Songea" alisema Mukugenzi huyo.

Posted by Unknown on 10:43 AM. Filed under , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0. Feel free to leave a response

Blog Archive

Labels

Recently Commented

Recently Added