ALBAM YA WEUSI YAKWAMA
Staa wa hip hop kutoka 'Kruu' ya Weusi iliyokita kambi pande za A-Town, Nikki wa Pilli amesema kuwa albam ya kundi hilo iliyokuwa itoke mapema mwezi uliopia imekwama.
Akizungumza na teentz.com mapema leo Nikki anayepewa heshima ya kuwa mmoja wa mastaa wa muziki huo wenye uwezo wa kuandika mistari mikali alifunguka kuwa kukwama kwa albamu hiyo kumekuja kufuatia matatizo ya kiufundi baada ya waliokuwa wakisimia kukamilika kwake kushindwa kuambatanisha moja ya wimbo katika uliokuwa ndani ya albam hiyo baada ya kufutika kutoka katika kumbukumbu za komputa.
"Ni jambo ambalo limetusikitisha hata sisi kwa kuwa tulikuwa tunajuwa kuwa mashabiki wetu wanahitaji albam hiyo, wimbo mmoja umefutika ndiyo sababu kubwa ya kukwama kutoka lakini hata hivyo fans wetu wasiwe na wasi wasi kwani tayari tatizo hilo limeshughulikiwa na soon tutawatangazia tarehe ya kutoka tena kwa mzigo huo" alisema Nikki.