|

Aibu tupu Miss Apanda Jukwaani Bila Kufuli


Ni aibu tupu! Mnyange aliyeibuka mshindi wa pili kwenye kipute cha Miss Vyuo Vikuu au Miss Higher Learning 2012/13, Fatma Ramadhan (pichani), ameacha gumzo baada ya kukwea jukwaani akiwa kaacha wazi mlango wake wa ‘ikulu’ bila kufuli, Risasi Jumamosi linairusha hewani.
NI MBELE YA MBUNGE
Tukio hilo la aina yake lililoshuhudiwa na mwandishi wetu, lilijiri usiku wa kuamkia Julai 7, mwaka huu kwenye Ukumbi wa New Maisha uliopo Masaki, Dar es Salaam ambapo mgeni rasmi alikuwa ni Mbunge wa Kisesa kwa leseni ya CCM, Mhe. Luhaga Joelson Mpina.
Katika tukio hilo ambalo hata mheshimiwa mbunge aliliona na kutazama pembeni, ilifahamika kuwa mrembo huyo aliyetimba jukwaani akiwa hajavaa nguo ya ndani, alitokea kwenye Chuo Cha Uandishi wa Habari mkoani Arusha.
“Jamani… jamani! Yaani huyu binti yuko uchi kabisa, imekuwaje au kajisahau? Ni aibu iliyoje, tena mbele ya mheshimiwa mbunge? Hii kweli aibu tupu,” alisikika mmoja wa watazamaji wa kinyang’anyiro hicho.
RASHIDA NAYE AANIKA MAMBO
Katika tukio lingine la aibu kwenye ‘iventi’ hiyo, kivazi cha mkufunzi wa warembo ambaye ni Miss Mara 2000, Rashida Wanjara kiliacha watu midomo wazi baada ya kuanika mambo yake nyeti ya mwilini.
“Duh! Huyu naye kiboko. Yaani kila kitu mpaka vya chumbani kaviacha hadharani?”
HEBU MSIKIE
Risasi Jumamosi lilipomvaa na kumuuliza kulikoni kuvaa kigauni kinachoonesha maungo yake nyeti, alifunguka: “Mimi ndiye miss nisiyechuja, nikiamua kushiriki umiss bado nakubalika na mwili wangu unalipa.”

Posted by Unknown on 9:43 PM. Filed under , . You can follow any responses to this entry through the RSS 2.0. Feel free to leave a response

Blog Archive

Labels

Recently Commented

Recently Added